Kiswahili

Home
Up
Topic 1
Topic 2
Topic 3
Topic 4
Topic 5
Topic 6
Topic 7
Topic 8

SILABI YA KISWAHILI YA KIDATO CHA 5 

Mukhtasari huu umeandikwa kwa kuzingatia matokeo ya tathmini ya muhtasari wa 1976 iliyofanywa na Taasisi ya  ukuzaji Mitaala mwaka 1988. Mapendekezo hayo yalitokana na upimaji wa uwezo wa wanafunzi na maoni  ya waalimu na wakaguzi. 

Mada za mukhtasari huu zimepangwa kulingana na vidato. Inashauriwa mada hizi zifundishwe kwa njia ya kuchanganya na si kwa kufuata mtiririko wa mada uliomo kwenye muhtasari huu. Kwa mfano, katika wiki moja, mwalimu anaweza kufundisha  vipengele vya fasihi simulizi kwenye kipindi kimoja, vya sarufi kipindi kingine na vya utungaji katika  vipindi vingine.

 Mwalimu anashauriwa kuzingatia yafuatayo

  1. Pamoja na njia/mbinu za kufundishia zilizoandikwa humu, mwalimu abuni njia nyingine kulingana na uwezo na  vionjo vya wanafunzi wake.
  2. Atengeneze na kutumia vifaa vya kufundishia kulingana na mahitaji ya wanafunzi wake.
  3. Ajielemishe  kwa kusoma maandiko mbalimbali yanayochapishwa kila wakati.
  4. Awe mfano mzuri wa kuzungumza na kuandika Kiswahili fasaha.
  5. Orodha ya vitabu vya kufundishia Kiswahili itakuwa ikitolewa na Wizara ya Elimu kila  baada ya muda maalum.
  6. Muhtasari huu unahitaji vipindi kumi na viwili kwa wiki.

 Malengo ya kufundisha kiswahili katika shule za Sekondari

Mafunzo ya Kiswahili katika shule  za Sekondari yanakusudiwa  kuwawezesha wanafunzi

  1. Kutumia Kiswahili kwa ufasaha katika fani zote za maisha
  2. Kuhakiki kazi za fasihi ya Kiswahili
  3. Kujenga tabia ya udadisi katika masuala ya lugha ya Kiswahili
  4. Kuelewa kuwa Kiswahili ni sehemu muhimu ya Utamaduni wa Tanzania

Malengo ya Kidato  cha Tano

Wanafunzi waweze:

  1. Kufafanua chimbuko la Kiswahili
  2. Kueleza ukuaji na ueneaji wa kiswahili
  3. Kufafanua nadharia ya fasihi
  4. Kujadili dhima ya udhamini wa kifasihi
  5. Kujadili nadharia ya uhakiki wa kifasihi
  6. Kufafanua tanzu za fasihi simulizi
  7. Kujadili mbinu za kifani katika fasihi simulizi
  8. Kujadili ukuaji wa fasihi simulizi
  9. Kujadili uhifadhi wa fasihi  simulizi
  10. Kuhakiki fasihi simulizi
  11. Kutunga kazi za fasihi simulizi
  12. Kufafanua tanzu za fasihi andishi
  13. Kujadili mbinu za  kifani  katika  fasihi andishi
  14. Kujadili ukuaji wa fasihi andishi
  15. Kuhakiki  kasi za fasihi andishi
  16. Kutathmini mitazamo ya wanafasihi
  17. Kutunga kazi za fasihi andishi
  18. Kutambua kauli ya Kiswahili
  19. Kubainisha virai na vishazi
  20. Kueleza  muundo wa ngeli
  21. Kuchanganua sentesi kwa njia ya  mishale na  maelezo
  22. Kujibu maswali ya ufahamu
  23. Kujadili mada anuwai
  24. Kutumia taratibu za uandishi
  25. Kutumia lafudhi ya Kiswahili
  26. Kuandika insha, simu, mialiko na barua
  27. Kutambua mitindo anuai katika kuzungumza na kuandika
  28. Kutambua mbinu za kifani katika kuzungumza na kuandika
  29. Kueleza dhima za mbinu za kifani
  30. Kutathmini matumizi ya semi na tamadhali
  31. Kutambua makosa ya kisarufi na kimantiki
  32. Kusahihisha makosa ya kisarufi  na kimantiki

MADA

  1. HISTORIA YA KISWAHILI
  2. FASIHI KWA JUMLA
  3. FASIHI SIMULIZI
  4. FASIHI ANDISHI
  5. SARUFI
  6. UFAHAMU NA UFUPISHO
  7. UTUNGAJI
  8. UTUMIZI WA LUGHA

 

 

Home ] Up ] News ] Subject O Level ] Subjects A level ] Services ] Profile ] Contact ]

Send mail to compeddie2000@hotmail.com  with questions or comments about this web site.
Copyright © 1998 ISSAM INTERNATIONAL