Kiswahili

Home
Up
Topic 1
Topic 2
Topic 3
Topic 4
Topic 5
Topic 6
Topic 7

SILABI YA KISWAHILI YA KIDATO CHA 6

Mukhtasari huu umeandikwa kwa kuzingatia matokeo ya tathmini ya muhtasari wa 1976 iliyofanywa na Taasisi ya  ukuzaji Mitaala mwaka 1988. Mapendekezo hayo yalitokana na upimaji wa uwezo wa wanafunzi na maoni  ya waalimu na wakaguzi. 

Mada za mukhtasari huu zimepangwa kulingana na vidato. Inashauriwa mada hizi zifundishwe kwa njia ya kuchanganya na si kwa kufuata mtiririko wa mada uliomo kwenye muhtasari huu. Kwa mfano, katika wiki moja, mwalimu anaweza kufundisha  vipengele vya fasihi simulizi kwenye kipindi kimoja, vya sarufi kipindi kingine na vya utungaji katika  vipindi vingine.

 Mwalimu anashauriwa kuzingatia yafuatayo

  1. Pamoja na njia/mbinu za kufundishia zilizoandikwa humu, mwalimu abuni njia nyingine kulingana na uwezo na  vionjo vya wanafunzi wake.
  2. Atengeneze na kutumia vifaa vya kufundishia kulingana na mahitaji ya wanafunzi wake.
  3. Ajielemishe  kwa kusoma maandiko mbalimbali yanayochapishwa kila wakati.
  4. Awe mfano mzuri wa kuzungumza na kuandika Kiswahili fasaha.
  5. Orodha ya vitabu vya kufundishia Kiswahili itakuwa ikitolewa na Wizara ya Elimu kila  baada ya muda maalum.
  6. Muhtasari huu unahitaji vipindi kumi na viwili kwa wiki.

 Malengo ya kufundisha kiswahili katika shule za Sekondari

Mafunzo ya Kiswahili katika shule  za Sekondari yanakusudiwa  kuwawezesha wanafunzi

  1. Kutumia Kiswahili kwa ufasaha katika fani zote za maisha
  2. Kuhakiki kazi za fasihi ya Kiswahili
  3. Kujenga tabia ya udadisi katika masuala ya lugha ya Kiswahili
  4. Kuelewa kuwa Kiswahili ni sehemu muhimu ya Utamaduni wa Tanzania

Malengo ya Kidato cha Sita

Wanafunzi waweze

  1. Kufafanua dhima ya vyombo  vya habari katika kukuza na kueneza kiswahili
  2. Kueleza maana na matumizi ya pijini,  lahaja na kreole
  3. Kueleza maana na matumizi ya lugha ya  kwanza, ya pili,  rasmi  na ya taifa
  4. Kujadili mbinu za kifani katik afsihi simulizi
  5. Kujadili ukuaji wa fasihi simulizi
  6. Kujadili uhifadhi wa fasihi simulizi
  7. Kuhakiki kazi za fasihi simulizi
  8. Kutunga kazi za fasihi simulizi
  9. Kuhakiki kazi za fasihi andishi
  10. Kufafanua maana matumizi na mipaka ya uhuru wa mwandishi
  11. Kuhakiki misimamo ya waandishi
  12. Kufafanua aina za  maneno
  13. Kufafanua matumizi ya  ngeli
  14. Kuchanganua sentesi kwa njia za matawi, majedwali, maelezo na mishale.
  15. Kujibu mswali ya ufahamu
  16. Kubainisha mawazo makuu
  17. Kutathmini habari
  18. Kujenga hoja
  19. Kuandika insha, risala, hotuba, matangazo na barua
  20. Kutambua mitindo ya uzungumzaji na uandishi
  21. Kutumia sanaa ya uzungumzaji hadharani
  22. Kuhakiki fani katika fasihi
  23. Kutambua makosa ya kisarufi na kuyasahihisha
  24. Kujadili dhima ya rejesta katika lugha.

MADA

  1. HISTORIA YA KISWAHILI
  2. FASIHI SIMULIZI
  3. FASIHI ANDISHI
  4. SARUFI
  5. UFAHAMU NA U FUPISHO
  6. UTUNGAJI
  7. UTUMIZI WA LUGHA
 

Home ] Up ] News ] Subject O Level ] Subjects A level ] Services ] Profile ] Contact ]

Send mail to compeddie2000@hotmail.com  with questions or comments about this web site.
Copyright © 1998 ISSAM INTERNATIONAL